Imani Na Uinjilishaji Ndio Msingi Wa Kanisa

2025-06-29
Dominika Ya 13 Ya Mwaka: Sherehe Ya Watakatifu Petro Na Paulo
Pd. Nicas Mrosso, OFMCap.
📖 Masomo ya Dominika

Somo la Kwanza: Mdo 12:1-11; 2

Somo la Pili: Tim 4:6-8, 17-18

Injili: Mt 16:13-19

🕊️ Tafakari ya Neno

 

Watakatifu Petro na Paulo ni nguzo mbili za kanisa waliojitoa kwa dhati kueneza kazi Kristo baada ya ufufuko. Ndio waliosia mbegu ya ukristo katika kanisa la mwanzo. Walifuata Njia ya Uzima, waliiungama ukweli, na wakaufia ukweli.

 

  1. PETRO: Aliitwa Simoni mwana wa Yona (Mt 16:17 a), alikuwa mkazi wa Bethsaida kando ya ziwa Galilaya. Alikuwa na familia. Yeye pamoja na nduguye Adrea walikuwa wavuvi. Hadi hapo Bwana alipomwita na kumfanya kuwa mvuvi wa watu. Anajulikana pia kama Kepha, kwa kiaramayo “Mwamba”. Baada ya kumkiri Yesu kuwa Kristo, Yesu alimkabidhi funguo za ufalme wa Mbingu. Alikabidhiwa mamlaka kwamba lolote atakalolifunga duniani na mbinguni linafungwa na lolote atakalolifungua duniani na mbingun litakuwa limenguliwa. Hivyo Petro alipokea mamlaka ya kuliongoza kanisa kutoka kwa Kristo.
  2. PAULO: Naye aliitwa na Yesu kuwa mtume wa mataifa. Tofauti na mitume wengine, Paulo alichaguliwa na Yesu baada ya Ufufuko. Mtu aliyekuwa wa imani kali ya kiyahudi. Alikuwa myahudi na myunani pia.  Alifanya mageuzi ya kweli alipokutana na Yesu Mfufuka. Baada ya Kuongoka alieneza habari njema kwa ari, ujasiri na kujitoa. Barua alizoandika ndizo zinazosoma hadi leo katika Biblia. Aliijjiita mtumwa (Rum 1:1), mdogo katika mitume, (1 Kor 15:9), hata kuliko watu wote (Efe 3:8).

Mtakatifu Petro ni mfano wa uongozi kiimani na mwamwinifu kwa wito wake wa kulichinga kanisa.

Mtakatifu Paulo ni mfano wa ujasiri wa kutangaza Injili, hata kwa gharama ya Maisha.

Watu wanaojitolea kuongoza na kutumikia bila kujitafutia faida binafsi. Bila kuogopa mateso. Wanaotenda kwa imani kubwa.

Kwa pamoja sasa Petro na Paulo, kanisa la mwanzo lilisimikwa imara na likaenea pande zote za dunia. Hakuna kinachoweza semwa kwa kuanzishwa kwa kanisa la Kristo, baada ya Kristo, pasipo miamba hii miwili. Damu yao iliyomwagika inasema zaidi, na sisi tuliokusanyika hapa ni matunda ya Imani yao na ushuhuda wao kwa Kristo.

     Tunaposherekea ushindi wao, tunaalikwa kuiga na kupenda Imani yao, maisha yao, majaribu yao, mateso yao, mafundisho yao, na kuwa miamba ya kanisa ya wakati wetu kwa kuusimamia ukweli na kuufundisha.